advanced Search
KAGUA
7731
Tarehe ya kuingizwa: 2010/11/09
Summary Maswali
je ni wajibu wangu kulipa fidia ya funga zilizonipita kwa kutokana na uzembe wa wazazi wangu?
SWALI
mimi ni kijana niliyelelewa katika familia isiyojaji dini, hali ambayo imenifanya mimi kuwa si mwenye kufunga tokea nikiwa na umri wa miaka kumi na tano, niakaendela kubakia katika hali hiyo kwa muda wa miaka minanae, na nilianza kuzifahamu sheria za dini pale nilipofikia umri wa miaka ishirini na nne, na hapo ndipo nilipoanza kufunga, na hivi sasa nimeamua kuzilipa zile funga za miaka minane iliyopita, je ni wajibu wangu pia kuzilipia fidia funga hizo? Nataraji kupata ufafanuzi wa kutosha kutoka kwenu, nakushukuruni sana na ahsanteni sana.
MUKHTASARI WA JAWABU

Ofisi ya Ayatullahi Sistani (Mungu ameweke) inajibu kwa kusema:

Iwapo wewe ulikuwa hujui kuwa saumu ni wajibu, basi lipa tu hizo funga za miaka minane, na hakuna haja ya kuzilipia fidia.

 

Ofisi ya Ayatullahi Makaarim Shiraziy (Mungu amuweke) nayo inajibu kwa kusema:

Anza kuzilipa sala na funga kidogo kidogo, na kuhusiana na ulipaji wa fidia juu ya funga hizo, rejea katika kitabu chetu Taudhihul-masaail, kwenye suala la 1401 hadi 1402, na lile ambalo litakuwa liko nje ya uwezo wako, Mola atakusamehe.

 

Ofisi ya Ayatullahi Safi Gulpeigani nayo iasema:

Iwapo utakuwa wewe ulikuwa ukijua kuwa saumu ni wajibu kwa yule aliyefikia baleghe, kisha ukawa unajuwa kuwa mwanzo wa baleghe ni kuanzia umri gani, hapo utawajibikiwa kuzilipia fidia saumu hizo pamoja na kuzikidhi.

 

Jawabu kutoka kwa Ayatullahi Mahdiy Hadawiy Tehraniy (Mungu amlinde):

Hukumu ya mtu ailyekula kwa makusudi, ni kufunga siku sitini mfullulizo au kuwalisha mafakiri sitini kwa kila siku moja ambayo umekula. Iwapo mtu atataka kutoa kafara (fidia) ya funga ya siku moja, itambidi ampe fakiri kiwango cha gramu 750 za chakula, kama vile ngano, mchele au kile chenye kufanana na vitu kama hivyo.

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI