advanced Search
KAGUA
13827
Tarehe ya kuingizwa: 2012/04/10
Summary Maswali
ndani ya vitabu vya fiqhi katika ibara inayohusiana na utoharikaji na usafikaji wa vitu kamavile kuta, majengo pamoja na ardhi, kumeandikwa ibara isemayo: ili jua liweza kuitoharisha na kuisafisha ardhi au kuta za jengo fulani kutokana na najisi fulani, inabidi zizingatiwe sharti maalumu, nazo ni kwamba: hakutakiwi kuwepo kuzuizi juu ya ardhi ua kuta ziliyonajisika, wala hakutakiwi kuwepo uwazi wenye kupitisha hewa baina ya tabaka la juu lililonajisika na lile tabaka la ndani lililonajisika…, naomba munifahamishe, nini maana hasa ya ibara hii? Tafadhalini nifafanulieni kwa uwazi kabisa.
SWALI
ndani ya vitabu vya fiqhi katika ibara inayohusiana na utoharikaji na usafikaji wa vitu kamavile kuta, majengo pamoja na ardhi, kumeandikwa ibara isemayo: ili jua liweza kuitoharisha na kuisafisha ardhi au kuta za jengo fulani kutokana na najisi fulani, inabidi zizingatiwe sharti maalumu, nazo ni kwamba: hakutakiwi kuwepo kuzuizi juu ya ardhi ua kuta ziliyonajisika, wala hakutakiwi kuwepo uwazi wenye kupitisha hewa baina ya tabaka la juu lililonajisika na lile tabaka la ndani lililonajisika…, naomba munifahamishe, nini maana hasa ya ibara hii? Tafadhalini nifafanulieni kwa uwazi kabisa.
MUKHTASARI WA JAWABU

Ufafanuzi juu ya swali lako ni kwamba: jua ni moja kati ya vitu vyenye kutoharisha, na miongoni mwa vitu vyenye kutoharishwa na jua ni: ardhi pamoja na kuta za nyumba.[i]

Ili jua liweze kutoharisha ardhi na pamoja na zile kuta za nyumba zilizonajisika, ni lazima kuwe hakuna kizuizi juu ya ardhi au kuta hizo wala ndani ya kuta hizo, kwa mfano iwapo kuta au ardhi itakuwa imenajisika na najisi hiyo ikawa imepenya hadi ndani ya ardhi au kuta hiyo, basi iwapo kwa njia moja au nyengine, kukawa kumewekwa kuzuizi kitachoigawa ardhi au kuta hiyo katika tabaka mbili, na kizuizi hicho kikawa kati na kati ya tabaka mbili hizo za ardhi au kuta, katika hali kama hiyo kuta na ardhi hiyo itatoharika sehemu ya tabaka la juu tu, na tabaka la chini litabakia kuwa ni najisi. Pia ili jua liweze kutoharisha, basi hakutakiwi kuwepo kizuizi juu ya ukuta au ardhi kama vile pazia au bao fulani. Vile vile iwapo kwenye ardhi au kuta kutapatikana uwazi utakao igawa sehemu mbili kuta au adrhi hiyo, huku uwazi huo ukawa kati na kati baina ya sehemu mbili zilizo najisika, yaaani sehemu ya nje na ya ndani, basi uwazi huo utazuia juwa lisiweze kuitoharisha ile sehemu ya ndani ya kuta au ardhi hiyo iliyonajisika.[ii] Lakini pia wanazuoni wengine hawakuzitaja sharti kama hizi katika ufafanuzi wao juu ya hali ya jua katika kuvitoharisha vitu kama hivyo.[iii] Pia kuna wanazuoni wengine wanaoamini kuwa: jua haliwezi kuzitoharisha kuta za nyumba.[iv]

 


[i] Taudhihul-Masaaili cha sayyid Ruhu-Llahi Khomeiniy kilichohakikiwa na kusahihihshwa na Sayyid Muhammad Husein Bani Haashimiy Khomeniy, juz/1, uk/117, chapa ya nane ya Intishaaraat Islaamiy, mwaka 1424 Shamsia.

[ii] Rejea rejeo lililopita, uk/118.

[iii] Rejea rejeo lililopita, uk/117 hadi uk/118, chini ya suala namba 191.

[iv] Miongoni mwa wanazuoni hao ni Ayatu-Llahi Makaarim Shirazi, yeye anasema kuwa: juwa huwa linatoharisha ardhi pamoja na mapaa ya nyumba, lakini si jambo lenye yakini kuwa jua ni lenye kutoharisha kuta pamoja na milango ya nyumba au madirisha. Angalia kwenye kitabu kiitwacho: Taudhihul-Masaaili, kilichoshereheshwa na Imamu Khomeiniy, juz/1, uk/118.

 

JAWABU KWA UFAFANUZI

Kwa ajili ya kupata ufafanuzi zaidi, rejea viungo na link zifuatazo kwenye tovuti yetu:

1- Swali la 4805: jua na utoharikaji wa nguo, mabrangeti na mazulia yaliyonajisika. Namba ya swali kwenye tovuti ni (5249).

2- Swali la 5002: sharti za kutoharika kwa kuta zilizonajisika kupitia jua. Namba ya swali ndani ya tovuti ni (5259).

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MASWALI KIHOLELA

  • Nini maana ya Feminism?
    15340 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Neno (Feminism) linatokana na lugha ya Kifaransa ambalo asili yake ya Kilatini ni (Femind), neno hili hutumika katika lugha mbali mbali huku likiwa na maana moja inayomaanisha uke au jinsia ya kike, ijapokuwa neno hili linapotumika kutoka lugha moja kwenda nyengine huonekana kuwa na mabadiliko kidogo ya ...
  • jee mwanaadamu ni mwenye uhuru katika matendo yake? Na kama yeye ni mwenye uhuru, basi mipaka ya uhuru wake ikoje?
    8618 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Mara nyingi mwanaadamu akiwemo katika msafara wa maisha yake binafsi, hujikuta akiwa ni mpweke na mgeni ndani ya msafara huo. Lakini hakuna budi kila mmoja wetu kuwemo ndani ya msafara huo. Ukiizingatia vizuri njia ya msafara wako, utaikutia kuwa: ndani yake huwa mna mambo yaliyokuwa tayari yameshathibitika ...
  • je dini na siasa ni vyenye kuendana au vyapingana?
    12715 Elimu mpya ya Akida 2012/05/23
    Dini ni chombo maalumu kilichokuja kumkomboa mwanaadamu na kumuongoza katika njia ya mafanikio, hivyo basi ni jambo lisiloingia akilini kuwa chombo hichi kiwe ni chenye kulipa mgongo jambo muhimu linalohitajika ndani ya jamii mbali mbali, kama vile suala la usimamishaji wa serikali. Na kwa upande mwengine ni ...
  • je majini na Malaika walikuja kumsaidia Imamu Husein (a.s) pale alipokuwa vitani huko Karbala? Na kama wao walikuja kumsaidia, basi kwa nini yeye aliukataa msaada huo?
    12225 تاريخ بزرگان 2012/05/23
    Kuna baadhi ya Riwaya na Hadithi zilizopokelewa kutoka kwa baadhi ya Maimamu (a.s) zenye kuashiria suala hilo. Lakini hakuna ajabu kuhusiana na suala hilo, kwani Mwenye Ezi Mungu aliwanusuru mitume tofauti pamoja na mawalii wake kwa kuwapelekea msaada wa majini na Malaika, kwa hiyo hilo ...
  • nini maana ya neno (dini)? Au dini hasa ni kitu gani?
    51120 Falsafa ya Dini 2012/05/23
    Wamagharibi wametumia ibara mbali mbali ili kupata maana muwafaka inayowafikiana na neno (dini), na neno (dini) ndani ya Qur-ani limetumika huku likibeba maana mbili tofauti, nazo ni kama ifuatavyo: 1- dini ni aina yeyote ile ya itikadi yenye kulenga nguvu maalumu za ghaibu zinazoaminiwa na ...
  • je Imamu Huein (a.s) aliwahi kuwa na bint aliyeitwa Ruqayya?
    7925 تاريخ بزرگان 2012/05/23
    Katika tokeo muhimu la Karbala, kulikuwa kuna aina nyingi za nyuso zilizong’ara, na baadhi ya nyuso hizo zilikuwa ni nyuso za watoto wadogo, lakini Tarehe haikunukuu habari kamili kuhusiana na nyuso zote za watoto hao. Lakini mmoja miongononi mwa watoto waliotajwa na Tarehe, ni Ruqayya mwana wa ...
  • Vipi mtu anaweza kuwa kipenzi cha Mwenye Ezi Mungu?
    7149 Tabia kimatendo 2019/06/16
    Katika lugha ya Kiarabu, -ambayo ndiyo lugha ya sheria ya Kiislamu- neno (pendo) linatokana na neno "حب". Ambalo lina maana ya kule mtu kuwa na mapenzi na mtu, kitu au jambo fulani. Lakini neno pendo, mapenzi au neno jengine lenye maana kama hii, linapotumika na kunasibishwa ...
  • hivi mvuta sigara aweza kuvuta sigara hali akiwa amefunga?
    7247 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Wanazuoni wote wa Kifiqhi wanasema kuwa: ni wajibu wa kila mwenye funga kuchukuwa tahadhari, na kutofikisha kitu chochote kile kama vile tumbaku au moshi wa sigara ndani ya koo yake.[1] Na hakuna hata mmoja miongoni mwa wanazuoni aliyetoa ruhusa ya kuvuta sigara ...
  • Batasan pakaian bagi perempuan untuk mengerjakan salat
    6428 Sheria na hukumu 2015/04/18
    Batasan wajib menutup aurat bagi perempuan adalah menutup seluruh badan termasuk rambut kecuali wajah (seukuran dengan basuhan ketika berwudhu), kedua telapak tangan dan kedua kaki sampai pergelangannya. Dari sisi ukuran kainnya, maka kain itu harus bisa menutupi badan artinya seukuran dengan badan dan rambutnya tidak kelihatan. ...
  • je ni wajibu wangu kulipa fidia ya funga zilizonipita kwa kutokana na uzembe wa wazazi wangu?
    7712 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Ofisi ya Ayatullahi Sistani (Mungu ameweke) inajibu kwa kusema: Iwapo wewe ulikuwa hujui kuwa saumu ni wajibu, basi lipa tu hizo funga za miaka minane, na hakuna haja ya kuzilipia fidia. Ofisi ya Ayatullahi Makaarim Shiraziy (Mungu amuweke) nayo inajibu ...

YALIYOSOMWA ZAIDI