advanced Search
KAGUA
8185
Tarehe ya kuingizwa: 2010/08/15
Summary Maswali
nini hukumu ya msafiri aliyefunga, ambaye atasafiri kabla au baada ya kuingia Adhuhuri?
SWALI
Kuna njia gani ya kuifanya funga ya yule anayesafiri baada ya adhuhuri kuwa ni salama, je hivi yeye atatakiwa kurudi kabla ya adhana ya asubuhi, au anaweza kubakia hadi hadi kabla ya kuingia adhana ya adhuri ya siku ya pili?
MUKHTASARI WA JAWABU

1- safari itakayo fanywa baada ya adhuhuri huwa haiharibu funga, na funga ya siku hiyo itakuwa sahihi.[1]

2- na mtu ambaye yuko safarini kisha akaamua kurudi kwake kabla ya adhuhuri, au akaamua kwenda sehemu ambayo ana nia ya kuweka makazi yake hapo kwa muda wa siku kumi, na pia akawa amefika sehemu aliyoikusudia  kabla ya kuingia adhuhuri, huku mtu huyo akawa hakutenda tendo linalobatilisha funga, mtu huyo atatakiwa kuifunga siku hiyo, na funga yake ni sahihi.[2]

Kwa mfano: iwapo mtu ataondoka baada ya adhuhuri ya siku ya Jumamosi na kuelekea sehemu fulani, funga yake ya Jumamosi itakuwa ni sahihi,lakini iwapo yeye atataka kuifanya funga yake ya Jumapili pia kuwa ni sahihi, itambidi kurudi kwake au kuelekea sehemu ambayo anakusudia kuweka makazi ya yake kwa muda wa siku kumi kabla ya kuingia adhuhuri na atatakiwa kufika hapo kabla ya adhuhuri. Na funga yake itakuwa ni sahihi iwapo yeye atakuwa hakutenda tendo la kuibatilisha funga hiyo, na anatakiwa kutia nia ya kufunga baada ya kuwasili kwake, hapo funga yake itakuwa ni sahihi.

 

 


[1] Sherehe ya imam Khomeiniy  Taudhihul-masaaili, juz/1, uk/953, suala la 1721.

[2]   Sherehe ya imam Khomeiniy  Taudhihul-masaaili, juz/1, uk/954, suala la 1722, na uk/953, suala la 1721.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI