advanced Search
KAGUA
6455
Tarehe ya kuingizwa: 2018/01/24
Summary Maswali
Tafadhali naomba munieleweshe, nini maana ya hijja kilugha?
SWALI
Tafadhali naomba munieleweshe, nini maana ya hijja kilugha?
MUKHTASARI WA JAWABU
Hijja kilugha; Ni kukisudia na kukiendea kitu au jambo fulani.[1]
Neno hijja Kisheria na kitaalamu; Neno hijja kisheria ni lenye kuashiria aina maalumu ya ibada yenye kutendeka mahala maalumu, kwa mfumo na wakati maalumu. Ibada hii inatakiwa kutendeka katika nyumba maalumu ya Mwenye Ezi Mungu iliyopo Makkah. Ibada hii inatakiwa kufanyika kwa nia ya kujikaribisha na kujisogeza kwa Mola Mtukufu.[2]
Kuna fungamano kubwa baina maana ya neo hijja kilugha na kisheria (kitaalamu), kwani mtu mwenye kutaka kufanya ibada ya hijja ni lazima aikusudie na aiendee nyumba ya Mwenye Ezi Mungu (Kaaba) ilioko Makka.

Twataraji utaridhika na jawabu hii.
Ahsante.
 

[1] Rejea kitabu: Jamharatul Lughah/juz 2/ Uk 86/ cha Muhammad bin Hussein Ibnu Darid/ Chapa kwanza ya Darul I’lmi lilmalayiin Beirut. Rejea kitabu: Mu’jamu Maqayisil Lugha cha Ibni Faris /Juz 2/Uk 29/ Chapa ya kwanza ya Maktabatul Ii’lam Al-islami/ Qum Iran/ Chapa ya mwaka 1404 Shamsia. Pia kwa ufafanuzi zaidi, unaweza kurejea kamusi mbali mbali za lugha ya Kiarabu.
[2] Rejea kitabu: Al-qamusul Fiqhi Lughatan wa Istilaha/ Uk 76-77/ Cha Abu Jaibi Saa’di/ Chapa ya pili ya Damascus iliyochapwa na taasisi ya Darul Fikr. 
TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MASWALI KIHOLELA

  • Timsahın saxlanılması və digər ölkələrə satışına icazə varmı?
    7443 Sheria na hukumu 2014/05/22
    Təqlid olunan müctehidlərin cavabları bunlardır: Həzrət ayətullah Xamnei (Allah qorusun) Əti haram olan heyvanların saxlanılması və onun hətta, bu heyvanların ətlərinin yeyilməsini halal bilənlərə də satılması düzgün deyildir. Amma, aqillər nəzərində halal mənfəətə görə olsa məsələn, ətinin başqa ət yeyən heyvanlar üçün istifadəsi yaxud, dərisinin dəri sənətində ...
  • je kuutangaza mwezi ni jukumu la wanazuoni wote kwa ujumla, au ni jukumu tu la kiongozi (mwanafiqhi / kadhi) mkuu wa dini nchini?
    9326 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Fani ya Fiqhi iliyo katika nyanja za juu (iliyobobea), huwa inampa mtu uwezo maalumu wa kuzivua na kuziopoa hukumu kuu za kisheria kutoka katika machimbuko yake, ambayo miongoni mwayo ni zile ibara za Qur-ani na Hadithi takatifu, na jambo hilo (kuwa na uwezo wa kuziopoa hukumu) ni ...
  • kwa nini tuwe wakalidi (wafuasi)?
    7724 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Ruhusa ya kumfuata ulamaa maalumu katika matendo ya ibada za kila siku, inatakiwa kutolewa na akili ya mtu mwenyewe. Na wala ruhusa hiyo haingojewi kutoka kwa Maulamaa, huku kila mmoja akielewa umuhimu wa suala hili ndani ya maisha yake ya kila siku. Katika hali yakawaida, ...
  • hivi mvuta sigara aweza kuvuta sigara hali akiwa amefunga?
    7266 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Wanazuoni wote wa Kifiqhi wanasema kuwa: ni wajibu wa kila mwenye funga kuchukuwa tahadhari, na kutofikisha kitu chochote kile kama vile tumbaku au moshi wa sigara ndani ya koo yake.[1] Na hakuna hata mmoja miongoni mwa wanazuoni aliyetoa ruhusa ya kuvuta sigara ...
  • tafadhalini tupeni ufafanuzi kuhusu mapokezi na maandiko ya Ziara ya siku ya Ashura.
    10220 Elimu ya Hadithi 2012/05/23
    Rejeo mama na asili hasa zinazo aminika ambazo zimeyanukuu maandiko ya Sala na salamu (Ziara) za siku ya Ashura ni vitabu viwili, navyo ni: kitabu Kaamiluz-ziaaraat cha Jaa'far bin Muhammad bin Quulewaihi Qummiy, ambaye amefariki mwaka 348 Hijiria, na cha pili ni kitabu kiitwacho Misbaahul-mujtahid cha ...
  • jee mwanaadamu ni mwenye uhuru katika matendo yake? Na kama yeye ni mwenye uhuru, basi mipaka ya uhuru wake ikoje?
    8652 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Mara nyingi mwanaadamu akiwemo katika msafara wa maisha yake binafsi, hujikuta akiwa ni mpweke na mgeni ndani ya msafara huo. Lakini hakuna budi kila mmoja wetu kuwemo ndani ya msafara huo. Ukiizingatia vizuri njia ya msafara wako, utaikutia kuwa: ndani yake huwa mna mambo yaliyokuwa tayari yameshathibitika ...
  • Vipi mtu anaweza kuwa kipenzi cha Mwenye Ezi Mungu?
    7188 Tabia kimatendo 2019/06/16
    Katika lugha ya Kiarabu, -ambayo ndiyo lugha ya sheria ya Kiislamu- neno (pendo) linatokana na neno "حب". Ambalo lina maana ya kule mtu kuwa na mapenzi na mtu, kitu au jambo fulani. Lakini neno pendo, mapenzi au neno jengine lenye maana kama hii, linapotumika na kunasibishwa ...
  • nini hukumu ya kufuga njiwa ndani ya sheria za Kiislamu? Na nini msingi hasa wa hukumu hiyo?
    24596 Sheria na hukumu 2012/06/17
    Tukilitazama suala la kufunga njiwa kibinafsi, tutalikutia kuwa suala hili halina matatizo na ni halali. Lakini pale sisi tutapolimbatanisha suala hili na haki za majirani au wanajamii, hapo tunaweza kulipa picha ya uhalali au uharamu kwa jinsi hali za jamii mbali mbali zinavyolitazama suala hilo. Baadhi ya ...
  • Nini maana ya Feminism?
    15388 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Neno (Feminism) linatokana na lugha ya Kifaransa ambalo asili yake ya Kilatini ni (Femind), neno hili hutumika katika lugha mbali mbali huku likiwa na maana moja inayomaanisha uke au jinsia ya kike, ijapokuwa neno hili linapotumika kutoka lugha moja kwenda nyengine huonekana kuwa na mabadiliko kidogo ya ...
  • nini hukumu ya kupiga sindano ya nguvu au kutia maji ya nguvu (Intravenous injection) mwilini ndani ya Ramadhani?
    9982 Sheria na hukumu 2012/05/23
    Wanazuoni wamekhitalifiana kuhusiana na suala hilo. Kwa kupata jawabu tosha, ni lazima utuambie kuwa wewe ni mfuasi wa mwanazuoni gani? Ili tuweze kukupa jawabu makini zaidi. Kwa vyovyote vile mitazamo ya baadhi ya wanazuoni wetu ni kama iuatavyo: Bahjat (r.a) na Khameneiy (Mungu amuhifadhi), wanasema: ...

YALIYOSOMWA ZAIDI