advanced Search

بلاگ

Wajukuu hawa wawili wa Mtume (s.a.w.w) ni mabwana wenye utukufu juu ya vijana wote Peponi, haidhuru kuwa ndani ya Pepo watu wote watakuwa katika hali moja ya ujana, ama wao (Imamu Hasan na Husein (a.s)) ndio watakaong’ara zaidi katika wale vijana waliouwawa katika njia ya Mola, au wale waliofariki katika umri wa ujana wao, na hilo si lenye kuupiku ule utukufu wa Mitume na Mawalii wengine wa Mwenye Ezi Mungu juu ya watu wa Peponi.

Mitume na Maimamu (a.s), ni watukufu kuliko wote miongoni mwa watu wa Peponi, kwa hiyo wote kwa ujumla akiwemo Imamu Hasan na Husein (a.s), ni wenye utukufu zaidi kuliko wale watu wengine wa Peponi, lakini tusisahau kuwa: kila mmoja miongoni mwa Mitume, Maimamu na Mawalii wa Mwenye Ezi Mungu, ni mwenye sifa maalumu inayompambanua na wengine. Pale basi Fatima (a.s) anaposifika kwa sifa ya kuwa Yeye ni bibi mtukufu kuliko wanawake wote wa Peponi, au pale Mmoja wa Maimamu (a.s), anapopewa sifa ya kuitwa bwana wa wenye kusujudu, huwa haimaanishi kuwa Fatima (a.s) amewapita mawalii wote kwa utukufu, na wala Yule Imamu aliyeitwa bwana wa wenye kusujudu, huwa kauli hiyo haimaanishi kuwa Yeye (a.s) ni bwana tu wa wenye kusujudu, na si bwana wa wale wasiosujudu, bali kila mmoja miongoni mwao huwa ameshikama na jambo au sifa njema maalumu yenye kumsababishia yeye kupata sifa ya aina fulani.

Ingawaje yawezekana upotoshwaji uliopatikana ndani ya Taurati na Injili ilioko mikononi mwa waumini wa Kikristo, ukawa umeyafuta majina ya watukufu hao, [1] lakini bado kuna Hadithi zenye kuelezea kuwa majina hayo yalikuwa ni maarufu ndani ya vitabu hivyo, nao walikuwa wakijulikana kwa jina la Aalu Abaa (a.s), na ibara hii ilikuwa ikiwakusudia:

Kwa mujibu wa nukuu za baadhi ya Hadithi ni kwamba, majina ya matano ya Aali Abaa (a.s), yaani Aali wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambao ni: Ali, Fatima,Hasan na Husein, yametajwa ndani ya Taurati na Injili. Pia suala hilo linaonekana kuashiriwa ndani ya ile Hadithi yenye kunukuu majadilianao ya kielimu yalipita baina ya Imamu Ridha (a.s) na watu wawili, ambao ni Jaaliith ambaye ni miongoni mwa viongozi wa Kanisa, na Ra-asul-Jaaluut ambaye ni miongoni mwa wakuu wa Kiyahudi.

thawabu za aiara ya Imamu Husein (a.s)

Jumanne, 25 Agosti 2020

Uislamu ni dini ya matendo, na malipo ya matendo hayo yapo kwa Mola mwnyewe, na ujira bora zaidi juu ya matendo hayo humuangukia yule mwenye matendo yaliotimia zaida kiikhlasi, na Mola ndiye mlipaji bora kuliko walipaji wote, naye hatoupoteza ujiwa wa mtu yoyote yule miongoni mwa watendaji hao.[1] Kila nia ya mja juu ya matendo ayatendayo inapokamilika kiikhlasi, na kila mja apostahamili madhila na mitihani mbali mbali kwa ajili ya Mola wake, ndipo anapopata ujira mkubwa zaidi, na thamani yake huwa ni kubwa zaidi mbele ya Mola wake. Na msingi huo ndio uliowafanya mitume na Maimamu (a.s) kuwa na cheo kikubwa zaidi kuliko wengine mbele ya Mola wao. Imamu Husein naye (a.s) ambaye ni Imamu wa tatu wa Kishia, ni mtu mwenye cheo kikubwa mbele ya Mola wake.

Hongera kwa kuzaliwa kwa Imam kazem (as)

Jumatatu, 10 Agosti 2020

Hongera kwa kuzaliwa kwa Imam Hadi (as)

Jumanne, 04 Agosti 2020

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI