advanced Search
KAGUA
7192
Tarehe ya kuingizwa: 2010/01/23
Summary Maswali
kuna dalili yoyote ile inayothibitisha kuwa Shimru alimchinja Imamu Husein (a.s) kwa kisogoni?
SWALI
kuna baadhi ya watu wanaonukuu kuwa, Shimru alimkata kichwa Imamu Husein (a.s) kwa kisogoni, je kuna dalili yoyote ile kuhusiana na nukuu hizo? Kama kuda dalili kuhusiana na hilo, naomba munitajie kuwa dalili hiyo iko kwenye kitabu gani?
MUKHTASARI WA JAWABU

Suala hilo limenukuliwa kutoka sehemu tofauti:

1- Imenukuliwa katika maneno ya Zainab (a.s) yaliyosema: “Ewe Muhmmad (s.a.w.w), wanao wa kike wamefanywa kuwa ni mateka, na wanao wa kiume wameuwawa, na upepo unavuma juu ya miili yao, na huyo hapo Husein (a.s) yupo chini hali akiwa amekatwa kichwa kwa kisogoni…”[1]

2- Kutoka kwa Imamu Sajjaad (a.s) yamenukuliwa maeno yafuatayo: “Mimi ni mwana wa yule aliyekatwa kichwa kwa kisogoni…”[2]

3- Kuna maandiko yenye kunukuu aina za salamu anazozisoma Imamu Mahdi (a.s) pale anapomsalia na kumsalimia Imamu Husein (a.s), yasemayo: “Sala na salamu ziwe juu ya yule aliyechinjwa kupitia kisogoni kwake…”[3]

 


[1] Bihaaru-Anwaar cha Muhammad Baaqir Majlisiy, juz/45, uk/59, chapa yenye mijalada 110  ya Daarul-Wafaa, Beirut Lebanon, mwaka 1404 Hijiria, pia rejea kitabu (Al-luhuuf) cha Ibnu Taawuus, uk131, chapa ya Jihan Tehran, mwaka 1348 Shamsia, pia rejea kitabu (Al-Manaaqib) cha Ibnu Shahr Aashuub Mazandaraniy, juz/4, uk/113, chapa ya Allaama yenye mijalada minne, Qum Iran, mwaka 1379 Hijiria.

[2] Bihaarul-Anwaar, juz/45/ uk/175.

[3] Bihaarul-Anwaar, juz/98/ uk/318, Hadithi ya 8.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI