advanced Search
KAGUA
9022
Tarehe ya kuingizwa: 2009/09/14
Summary Maswali
je mababu na wana wa Maalik Ashtar walikuwa ni wapenzi na wanaumini wanao uunga mkono uongozi wa Ahlul-Bait (a.s)?
SWALI
je mababu wa Maalik Ashtar walikuwa ni waumini? Na je Maalik Ashtar alikuwa na mtoto? Na kama alikuwa naye, je mwanawe naye alikuwa ni muridi (mpenzi na mfuasi) wa Ahlul-Bait (a.s) au la?
MUKHTASARI WA JAWABU

Kwa kweli hakuna kitabu miongoni mwa vitabu maarufu vya Tarehe vyenye kutegemewa kilichozungumzia na kuthibitisha suala la hali halisi juu ya wazee wa Maalik Ashtar, bali tu kinachofahamika kuhusiana nao, ni kuwa wao ni watu wa makabila ya (Nukha’a) na (Mudh-haj) yalioko huko Yemen, lililothibitika ndani ya Tarehe ni kwamba, makabila haya yalikuwa ni miongoni mwa makabila ya mwanzo yaliyoukubali na kuuamini Uislamu.

Maalik Ashtar alikuwa na watoto wawili wa kiume, mmoja alijulikana kwa jina la Is-haaq na mwengine Ibrahim. Is-haaq alikuwa ni mfuasi wa Imam Husein (a.s) aliyemuunga mkono Imamu Husein (a.s) kwenye mapambano ya Karbala, na hatimae kuuwawa katika mapambano hayo, na Ibrahim naye alikuwa ni mfuasi wa Ahlul-Bait (a.s), naye alishiriki katika mapambano yaliyotekea katika vugu vugu la kutaka kulipiza kisasi cha mauaji ya Imam Husein (a.s), vugu vugu ambalo lilianzishwa na Mukhtari Thaqafiy, huku Ibrahim akiwa ni miongoni mwa makamanda wa kivita ndani ya tokeo hilo, yeye aliifanya kazi yake kwa vizuri pasi na woga, na wengi miongoni mwa majahili waliomdhulumu Husein (a.s) walipata jaza yao ya kifo kupitia mkononi mwa Ibrahim, na mmoja miongoni mwa majahili muhimu alioweza kuwateketeza, ni Ibnu Ziad, ambaye alikuwa ndiye shetani mkuu dhidi ya Imamu Husein (a.s). vitabu vya Tarehe vinaelezea kuwa, Ibrahim alikuwa na watoto watano, nao ni: Nuuman, Maalik, Muhammad, Qasim na Khuulaan. Na miongoni mwa watoto hao watano, wapo watoto wawili ambao walikuwa ni wapokezi wa Hadithi, mmoja wao akiwa ni Muhammad na wa pili akiwa ni Qaasim.

JAWABU KWA UFAFANUZI

Maalik bin Harith bin Abdu-Yaghuth bin Salma bin Rabia bin Harith bin Khuzaima bin Sa’ad bin Maalik bin Nukha’a, anatokana na koo mbili asili zilizo shujaa nazo ni Nukha' na Mudh-haj.[1] Yeye alizaliwa katika zama za kijahili kabla ya kuja kwa Uislamu,[2] ama kuhusiana na namna ya kusilimu kwake yeye mwenyewe au ukoo wake, ni moja ya mambo ambayo hayakufafanuliwa na vitabu vya Tarehe, na wala hakuna Hadithi au mfano wa Hadhithi uliolizungumzia suala hilo.[3] Baadhi ya waandishi wanakadiria kuwa yeye alisilimu pale Imamu Ali (a.s) alipokwenda Yemen kuutangaza Uislamu.[4] Kwani makabila mengi yaliukubali Uislamu na kusilimu makundi kwa makundi, kama vile kabila la Hamdaan, Nukha’a na Mudh-haj.

Katika zama za ukhalifa wa Abu Bakar, ukoo huu asili wa Kiarabu ulishika njia ya Sham (Siria) kisha ukaelekea Iraq kwenye mji maarufu ujulikanao kwa jina la (Kuufa), na hapo ndipo yakawa makazi ya kabila hilo, wao walizaliana na kukusanyika siku baada ya siku, hadi ukoo wao ukakua na kuota mizizi ndani ya mji huo. Kizazi cha maalik kilikua siku baada ya siku, na hatimae kizazi hicho kikazaa koo kubwa zilizojulikana kwa jina la (Banu Maalik), (Banu Ibrahim) n.k. Pia hadi leo kuna koo mbali mbali ambazo nasabu zake zinatokana na Maalik Ashtar, na miongoni mwa koo hizo ni Aalu Kaashiful-Ghitaa na Aalu Radhiy.

Imenukuliwa kutoka kwenye vitabu vya Tarehe kuwa, Maalik alikuwa na watoto wawili waliojulikana kwa majina ya Ibrahim na Is-haaq. Is-haaq alikuwa ni mfuasi mkereketwa wa Imamu Husein (a.s) ambaye alishika upanga katika vita vya Karbala baada tu ya kuuwawa kwa Habib bin Madhahir, na hatimae akauwawa katika vita hivyo.[5] Ibrahim alikuwa ni mtoto shujaa wa Maalik Ashtar, ambaye ni mpenzi na mfuasi shupavu wa Ahlul-Bait (a.s). Yeye alikuwa ni Shia madhubuti aliye makini kiimani na kimatendo, na hakufanana tu na baba yake kiimani na kimatendo, bali pia alifanana naye kimwili pamoja na sura.[6] Muandishi maarufu wa Tarehe ajulikanaye kwa umaarufu wa Dhahabiy, amenukuu kutoka kwa waandishi wa Tarehe wa madhehebu ya Kisunni akisema: “Ibrahim alikuwa ni shujaa kama baba yake aliyebobea sifa njema na alikuwa ni miongoni mwa watu watukufu”.[7] Ibrahim alishiriki mapinduzi muhimu yaliosimamishwa na Mukhtari Thaqafiy kwa nia ya kutaka kulipiza kisasi na kuwapandisha katika kiriri cha sheria  wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyengine katika mauwaji ya Imamu Husein (a.s). Ibrahim waliweza kuwatokomeza maadui wengi wa Ahlul-Bait (a.s) ambao walishiriki katika mauaji ya Karbala, na miongoni mwa wale walioteketea kupitia mkononi mwake, ni Ibnu Zaid ambaye alimteketeza ndani ya siku ya kumi ya mwezi wa Muharram ya mwaka 67 Qamaria.[8] Vitabu vya Tarehe vimenukuu kuwa Ibrahim alikuwa na watoto watano waliojulikana kwa majina yafuatayo: Nuumani, Maalik, Muhammad, Qaasim na Khuulaan. Miongoni mwa watoto hawa, mna wale watoto wawili ambao walikuwa ni wapokezi wa Hadithi, nao ni Muhammd na Qaasim.[9]

Kwa ajili ya utafiti zaidi rejea: kitabu (A’ayani Shia) cha Sayyid Muhsin Amin, juz/2, uk/200, Daarut-Ta’ariif lilmatbuua’at, Beirut Lebanon, mwaka 1406 Qamaria.

 


[1] Dairatul-Maarif Shial- A’amma cha  Muhammad Husein A’alamiyul-Haairiy, juz/16, uk/40, chapa ya pili ya Muasastul-A’alamiy lilmatbuua’at, Beirut, chapa ya mwaka 1413. Pia  kitabu A’ayanush-Shia cha Sayyid Muhsin Al-Amin, juz/9, uk/38, chapa ya Dairatul-Ma’arif lilimatbuua’at, Beirut , chapa ya mwaka 1403. Pia kitabu Maalik Ashtar Khutabihi wa Aaraihi, cha Qeisul-Attaar, uk/13, chapa ya kwanza ya Muasasatul-Fikril-Islamiy Iran ya mwaka 1412.

[2] Rejea kitabu Al-A’alaam cha Khairud-Diin Al-Rarkaliy, juz/5, uk/259, chapa ya kwanza ya Daarul-Ilm, Beirut.

[3] Rejea kitabu Maalik Ashtar cha Sayyid Muhammad Ridha Al-Hakim, uk/33, chapa ya kwanza ya Maktabatul-Haidariyya Qum Iran, ya mwaka 1427.

[4] Rejea kitabu Maalik Ashtar cha Muhammad Muhammadiy Ishtihardiy, uk/19, chapa ya pili ya Intishaaraat Peyam Aazaadiy Tehran, mwaka 1372.

[5] Rejea kitabu Maalik Ashtar cha Muhammad Muhammadiy Ishtihardiy, uk/188.

[6] Dairatul-Maarif Shial- A’amma cha  Muhammad Husein A’alamiyul-Haairiy, juz/2, uk/131.

[7] Seiru A’alaamin-Nubalaa cha Dhahabiy, juz/4, uk/35, chapa ya tisa ya Muasasatur-Risaala, Beirut, mwaka 1413.

[8] Rejea kitabu (Al-Kaamil fit-taariikh) imenukuliwa kutoka kwa Ali Munfarid Nadhariy katika kitabu Qissatu Karbala, uk/670, chapa ya sita ya Intishaaraat Suruur, Qum Iran, mwaka 1379.

[9] Rejea gazeti la Risaalat no:6054 la tarhe 16/10/85 Shamsia lililomtafiti Maalik Ashtar na Maisha yake.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • Vipi mtu anaweza kuwa kipenzi cha Mwenye Ezi Mungu?
    8835 Tabia kimatendo 2019/06/16
    Katika lugha ya Kiarabu, -ambayo ndiyo lugha ya sheria ya Kiislamu- neno (pendo) linatokana na neno "حب". Ambalo lina maana ya kule mtu kuwa na mapenzi na mtu, kitu au jambo fulani. Lakini neno pendo, mapenzi au neno jengine lenye maana kama hii, linapotumika na kunasibishwa ...
  • je mtu asiwajibikiwa kufunga (asiyefunga) ana ulazima wa kutoa zakatul-fitri?
    11954 زکات فطره 2012/05/23
    Mtu atakaeingiliwa na usiku wa Idil-fitri, huku akiwa ni baleghe na mwenye akili timamu, naye akiwa si mtumwa wa mtu wala si fakiri, mtu huyo atawajibika kutoa zakatul-fitri kwa ajili yake na kwa ajili ya wale wote anaowahudumia, na kiwango cha kila mmoja ni kiasi cha kilo ...
  • maadili mema yana nafasi gani kwenye uwanja wa mazoezi?
    12966 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Uisalmu ni dini kamili iliyokusanya ndani yake mfumo kamili na salama wenye kutoa muelekeo wa kiutendaji kuhusiana na kipengele kimoja kimoja miongoni mwa vile vipengele vinavyo husiana na maisha ya mwanaadamu. Uislamu haukuliweka nyuma suala la afya ya mwili wa kila mmoja wetu. Kwa hiyo Uislamu ni ...
  • kwa nini Uislamu unaamuru kuwanyonga wanaoritadi? Je hilo haliendani kinyume na uhuru wa kila mmoja kuabudu anacho kitaka?
    22870 حدود، قصاص و دیات 2012/05/23
    Kuritadi ni kitendo cha wazi kabisa cha kutoka katika dini, na mara nyigi tendo hilo hutumika kama ni nyenzo ya kuwadhoofisha wengine kiimani na kuwafanya waache dini yao, na hatimae kuwatoa na kuwaweka nje ya dini. Wanaohukumiwa hukumu ya kuritadi, ni wale wanaolidhihirisha tendo hilo kwa wengine, ...
  • nini maana ya itikafu
    21325 اعتکاف 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • je kitabu cha tarehe kijulikanacho kwa jina la Taarekhu-Tabari, ni kitabu kinachoaminika?
    10553 امام حسین قبل از امامت 2012/05/23
    Pale kitabu fulani kinaposemekana kuwa ni chenye kuaminika, huwa haimaanishi kuwa kila kilichomo ndani yake ni sahihi. Kitabu Taarikhut-Tabariy, si chenye kuepukana na usemi huu, bali nacho pia hakikubeba ndani yake yale yalio sahihi tu. La pili ni kwamba: kauli hiyo ulioinukuu kutoka katika kitabu hicho ...
  • je ni kweli kuwa Maimamu ni wabora zaidi kuliko hata Mitume?
    16934 دانش، مقام و توانایی های معصومان 2012/05/23
    Suala la Maimamu (a.s) kuwazidi Mitume katika daraja za kielimu, ni suala moja linalo onekana kuzungumziwa sana na Riwaya mbali mbali, na sababu hasa za wao kuwazidi Mitume kielimu, zinatokana na ule uhakika wa nuru ya maumbile yao, kwani uhakika wa nuru yao unatokana na uhakika wa ...
  • nini hukumu ya kufuga njiwa ndani ya sheria za Kiislamu? Na nini msingi hasa wa hukumu hiyo?
    26426 نگهداری و شکار حیوانات 2012/06/17
    Tukilitazama suala la kufunga njiwa kibinafsi, tutalikutia kuwa suala hili halina matatizo na ni halali. Lakini pale sisi tutapolimbatanisha suala hili na haki za majirani au wanajamii, hapo tunaweza kulipa picha ya uhalali au uharamu kwa jinsi hali za jamii mbali mbali zinavyolitazama suala hilo. Baadhi ya ...
  • Je ni kweli kuwa Imamu Husein (a.s) aliwahi kuwa na binti mwenye umri wa miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Sukaina anaye semekana kuwa alifariki dunia huko Damascus?
    11645 اهل بیت و یاران 2012/05/23
    Ingawaje wengi miongoni mwa waandishi wa Historia hawakukinukuu kisa cha kuwepo kwa mtoto huyo wa kike wa Imamu Husein (a.s) mwenye umri wa kiasi cha miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Fatimatu Sughra na baadhi ya wakati akijulikana kwa majina yasiokuwa hayo, lakini ...
  • je dini na siasa ni vyenye kuendana au vyapingana?
    14099 Elimu mpya ya Akida 2012/05/23
    Dini ni chombo maalumu kilichokuja kumkomboa mwanaadamu na kumuongoza katika njia ya mafanikio, hivyo basi ni jambo lisiloingia akilini kuwa chombo hichi kiwe ni chenye kulipa mgongo jambo muhimu linalohitajika ndani ya jamii mbali mbali, kama vile suala la usimamishaji wa serikali. Na kwa upande mwengine ni ...

YALIYOSOMWA ZAIDI